1 / 7

Tanzania Tuitakayo : Wajibu na Majukumu ya Asasi za Kiraia katika Kujenga Tanzania Tuitakayo

Tanzania Tuitakayo : Wajibu na Majukumu ya Asasi za Kiraia katika Kujenga Tanzania Tuitakayo . Maeneo yanayoangaliwa na Mada . TANZANIA TUNAYOITAKA BAADA YA MIAKA 50 YA UHURU WAJIBU NA MAJUKUMU YA ASASI ZA KIRAIA KATIKA KUIJENGA TANZANIA TUITAKAYO. Tanzania Tuitakayo.

laddie
Télécharger la présentation

Tanzania Tuitakayo : Wajibu na Majukumu ya Asasi za Kiraia katika Kujenga Tanzania Tuitakayo

An Image/Link below is provided (as is) to download presentation Download Policy: Content on the Website is provided to you AS IS for your information and personal use and may not be sold / licensed / shared on other websites without getting consent from its author. Content is provided to you AS IS for your information and personal use only. Download presentation by click this link. While downloading, if for some reason you are not able to download a presentation, the publisher may have deleted the file from their server. During download, if you can't get a presentation, the file might be deleted by the publisher.

E N D

Presentation Transcript


  1. Tanzania Tuitakayo: Wajibu na Majukumu ya Asasi za Kiraia katika Kujenga Tanzania Tuitakayo

  2. Maeneo yanayoangaliwa na Mada • TANZANIA TUNAYOITAKA BAADA YA MIAKA 50 YA UHURU • WAJIBU NA MAJUKUMU YA ASASI ZA KIRAIA KATIKA KUIJENGA TANZANIA TUITAKAYO

  3. Tanzania Tuitakayo • Uchumi endelevu unaotokana na juhudi za mtanzania mmojammoja ama kupitia ushirika ama makampuni yao. Uchumi endelevu ni ule ambao wananchi wake wanakuwa ni sehemu ya shughuli za uchumi badala ya kuwa watazamaji wa shughuli za uchumi- mfano wa Malesia- ilikuwa ni nchi maskini duniani wakati inapata uhuru wake miaka ya 60 kama sisi lakini chini ya Waziri wake Mkuu Mahatma Mohamed aliweza kubadilisha uchumi wa nchi hiyo kutoka kilimo cha mpira kwenda kwenye uchumi wa Viwanda (semi industrialized economy)

  4. Matumizi ya Rasilimali za nchi zinatumika kwa manufaa ya watanzania walio wengi • Ushiriki yakinifu wa wananchi katika kupanga mipango yao ya maendeleo – wakitumia vema zana ya O&OD • Jamii inayowawajibisha viongozi na watendaji waliowachagua -Viongozi na watendaji katika ngazi zote, Serikali Kuu, Serikali zaMitaa, Asasi za Kiraia • Usawa wa kijinsia katika ngazi mbalimbali za Maamuzi tukianzia na ngazi za juu hadi chini

  5. Mfumo wa Elimu ambao lengo lake kuu sio kumuandaa mtu kutafuta ajira bali elimu ya kumwezesha mtu kuyakabili vema mazingira yanayomzunguka kwa kutumia ujuzi alioupata shuleni/chuoni • Fursa sawa kwa wote na hasa makundi yanayoweza kusahaulika katika kuamua mustakabali wa Taifa letu • Uvumilivu wa kisiasa na demokrasia (Political &Democratic tolerance)-kutambua tofauti za kiitikadi miongoni mwetu, kusikilizana, kuheshimiana na kutambua mchango wa kila mmoja wetu katika kuendeleza nchi hii

  6. Miradi na Programu zinazotokana na Utafiti wa Uhitaji na ubaini wa matokeo chanya kwa nchi lakini pia kufanya tathmini ya athari za miradi mfanoathari zitokanazo na uchimbaji wa madini kama ureniamu • Huduma zilizo bora zaidi na upatikanaji wake ni rahisi kwa kila mtu • Mfumo wa utawala wenye tija na wenye maslahi kwa jamii- inawezekana tukitumia ipasavyo dhana ya Decentralization tutapunguza mzigo wa viongozi mfano wakuu wa Mikoa, Ma-RAS tukabakiza Wakuu wa Wilaya

  7. Majukumu na wajibu wa AzaKi • Kufanya tafiti zenye kubaini ukweli wa hali halisi katika nyanja zote ili kuiishauri vema serikali • Kutoa elimu kwa jamii hususan juu ya haki zao na wajibu wao • Kujenga uwezo wa jamii ili iweze kuiwajibisha Serikali pale inapohitajika • Kuishinikisha Dola pale ambapo mambo hayaendi sawa • Kutetea na kuhamasisha jamii kuhusu haki zao, masuala ya maendeleo, sera, sheria, ushiriki na ushirikishwaji, utawala bora na uwajibikaji

More Related